Monday, February 10, 2020

KUHUSU SEM-BT



Karibu sana mpenzi msomaji wangu na leo nakuletea utambulisho wa kikundi kidogo cha SEM-BT.

SEM-BT ni kikundi cha watu wachache ambacho kinatoa huduma zake hapa tanzania

Kikundi cha SEM BAND – TANZANIA (SEM-BT) ambacho kimesajiliwa kisheria kwa namba za usajili CDC/CSO/114/2019, ambacho makao makuu yake ni Chato kati karibu na ilipokuwa ofisi ya TANESCO, kinajishughulisha na shughuli  za kuandaa matamasha mbalimbali ya  uimbaji wa nyimbo ikiwa ni pamoja na kuziweka katika mfumo wa sauti na Video na kuuza DVD ili kujipatia kipato. Pamoja na kuwaunganisha vijana kuwa pamoja katika shughuli mbalimbali za kiuchumi, kidini na kijamii.

Kikundi hiki kilianzishwa tangu mwaka 2016 ambapo kilikuwa na watu wawili tu na kazi zake ilikuwa ni kuwaunganisha watu mbalimbali katika matamasha mbalimbali ya kidini na kijamii. kikundi hki hakikuweza kuendelea zaidi kutokana na kukosa pesa za kuendeshea kikundi. Mwaka 2019 waasisi wa kikundi hiki waliamua kushirikisha wadau wengine ili kuweza kurekodi na tulifanikiwa kurekodi nyimbo mbili kwa mfumo wa sauti na video pia (Nyimbo hizo ni ("Basi iweni na huruma" uliotungwa na E.Ogeda pamoja na "Tuwe na moyo wa majitoleo" uliotungwa na E.Nyanza). Mpaka sasa hivi tunajiandaa kuzisambaza hizo nyimbo zetu kwa njia ya you tube na mitandao mingine ya kijamii muda si mrefu. kaa tayari kuzipokea.

Endelea kutufuatilia kwani tutakuletea mambo mengi mazuri kwa siku zinazokuja.

Emmanuel. Shimbala
Katibu SEM-BT

No comments:

VITU KUMI HATARI KWA AJILI YA SAUTI YAKO.

Nakushukuru ndugu msomaji wangu kwa kuendelea kufuatilia makala hizi.  Nilikuwa naongea na  Tabibu kutoka Hospitali ya wilaya ya C...