Habari za leo ndugu msomaji wa SEM-BT?
Leo nitaongelea kuhusu faida za kuimba ambazo
zinamsaidia mtu kiafya.
Kwanza kabisa naomba nikueleze maana ya kuimba.
KUIMBA ni
kutoa sauti yenye ulinganifu, sauti hiyo inatakiwa kufuata mapigo ya ki muziki
na ni zaidi ya kughani. Zamani mababu zetu walikuwa wanaimba kwenye kazi
mbalimbali ili kurahisisha kazi yenyewe iliyokuwa ikifanyika, mpaka sasa watu
wengi huimba ili kuburudisha, kufundisha, kukosoa au kuelimisha kikundi fulani
cha watu.
Kuimba ni faida kwa mwimbaji kwani kuna faida
nyingi saana ambazo mwimbaji anazipata kama vile kuburudika, kuburudisha,
kuinjilisha, kuhamasisha, kufariji, kufurahisha n.k
Leo nitakueleza faida za kuimba ambazo
zinamsaidia mwimbaji kiafya, Faida zenyewe ni:
- Kuimba ni mazoezi. Unapoimba
unafanya mazoezi ambayo pia ni kinga kwa magonjwa mbalimbali yanayoweza
kumuathiri mtu ambaye hafanyi mazoezi. Mazoezi ambayo nayasemea hapa ni
Kupanua kiwambo (diaphragm), mwanakwaya anatumia nguvu nyingi sana wakati
anaimba ili kupanua mapafu na kiwambo. Hii itamsaidia mwimbaji ku zuia
magonjwa yanayoweza kuathiri mapafu kama vile kikohozi, mafua.
- Inasaidia kuboresha mfumo wa upumuaji mwilini kwani
msukumo wa damu utakuwa mkubwa ambapo ndani ya chembe za damu huwa kuna hewa
safi ya Oxygen ambayo husambazwa mwilini pote na chembe za damu katika
mzunguko.
- Inasaidia kupunguza mawazo. Hili liko
wazi kabisa kwa mwanakwaya au mwimbaji yeyote yule, ukiimba
unapunguza mawazo. Mtu mwenye mawazo anaweza kuugua hata magonjwa ya akili
na kisaikolojia.
- Husaidia kusimama vizuri. Mwimbaji huwa
ana staili yake ya kusimama ambapo kifua chake anakiweka mbele, mabega
yanakuwa yameinuka kidogo ili kumsaidia kutoa sauti, mgongo pia unakuwa
umenyooka vizuri. Hii inamsaidia kuufanya uti wa mgongo usijikunje. Kwa
hiyo mwanakwaya anapoimba kwa muda mrefu huwa na tabia ya kusimama kama
anataka kuimba na hivyo kumsaidia yeye kutunza na kukinga uti wa mgongo.
- Huimarisha mfumo wa kinga mwilini. (strengthen the
immunity system) Kwenye mwili wa binadamu
kuna kinga (protini) ambayo ina jina la kitaalamu ambalo ni
Immunoglobulins, kwa hiyo mtu anapoimba anafanya mazoezi (kama nilivyosema
hapo juu) na unapofanya mazoezi ina maana kwamba unaongeza kinga mwilini
tofauti na mtu ambaye amekaa tu bila kufanya mazoezi
Kwa ufupi sasa kuimba kuna faida kiafya, faida
zingine nimezitaja hapa chini ambazo ni:
- Kuimba nidawa ya asili ya mawazo (natural
annti-depresant)
- Kuimba kunapunguza mawazo kwa kiasi kikubwa sana (ni
dawa kwa mtu mwenye mawazo)
- Kuimba kunaongeza uwezo wa kufikiri na kuchukua maamuzi.
Faida za kuimba kwenye jamii.
- Kuimba humsaidia mtu kuongeza idadi ya marafiki.
- Kuimba kunamwongezea mtu kujiamini katika kila kitu
anachokifanya kwa faida yake na jamii kwa ujumla.
- Kuimba kunapanua wigo wa mawasiliano.
- Kuimba humsaidia mtu kuwa na hisia juu ya kile
anachokiimba.
- Kwa wanakwaya wa nyimbo za dini, kuimba kunamweka karibu
na Muumba wake.
Kwa leo naomba niishie hapo, nakutakia kila la heri katika
majukumu mbalimbali ya kujenga taifa na jamii yetu kwa ujumla. Nakuomba pia
uendelee kuka mkao wa kusubiria kazi ambayo tutaitoa hewani muda si mrefu, ni
nyimbo mbili ambazo tulizirecord kwa mfumo wa sauti na video.
Imeandikwa na;
SEM BAND TANZANIA
CHATO-GEITA TANZANIA
+255 762 176 662 au +255
756 446 979
E-mail:
sembandtanzania@gmail.com
No comments:
Post a Comment